Friday, 13 June 2014

Picha 4 za Uwanja wa Jamuhuri Dodoma usiku huu tayari kwa shughuli #TANZANIA #NAIAMINIA


Pale ambapo mastaa zaidi ya 100 wa Tanzania kwenye muziki na filamu pamoja na sehemu nyingine wamesafiri kutoka 88.5 Dar es salaam mpaka 104.4 Dodoma na kuziunganisha nguvu zao kwa ajili ya kuhakikisha wanakamilisha walichokianzisha….. yani kuizindua video yao ya wimbo wa miaka 50 (Tanzania @50) .

Kwenye rekodi za Tanzania, hii itakua mara ya kwanza kufanyika kwa tukio kubwa kama hili kutokana na level waliyoiweka, maandalizi, wageni waalikwa lakini pia njia ya maamuzi bora ya nguvu ya ushawishi kuwafikia Watanzania.
Kuanzia Diamond Platnumz, Mwasiti, Roma, Baba Level, Quick Rocka, Izzo B, Shilole, Mwana FA, Meninah, Linex, Mrisho Mpoto, Wema Sepetu na mastaa wengine mbalimbali watakutana na Watanzania wengine katika mkusanyiko usio na kiingilio Jamuhuri Stadium leo June 14 2014 saa nane mchana kuendelea kuusambaza upendo na uzalendo.

No comments:

Post a Comment