Sunday, 29 June 2014

#Dope aint dope if it aint @bangfellahz @bangfellahz @bangfellahz @bangfellahz
Very few available @ Tsh 25000 pata kitu yako
#WTBFB #Obey #Starz #LordzGang #BangFellahz #BangOrDie #Bang_Bang #familybuznez
Don make me pull out ma pistol #Bang


Saturday, 28 June 2014

        MTU KWAO(JASIRI HAACHI ASILI)
                 NAJIVUNIA KUZALIWA KILIMANJARO





Mkoa wa Kilimanjaro ni kati ya mikoa 26 za Tanzania. Makao makuu ya mkoa huu ni MoshiMlima wa Kilimanjaro, mlima mkubwa kupita yote barani Afrika umo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro. Jina la mlima huu ndio limeupatia mkoa huu jina lake.
Mkoa wa Kilimanjaro umepakana na Kenya upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa Kusini na mikoa ya Manyara naArusha upande wa magharibi.
Kilimajaro kuna wakazi wapatao 1,381,149 (sensa ya mwaka 2002). Makabila makubwa mkoani humo ni Wachagga naWapare ambapo pia kuna makabila mengine madogo madogo kamaWamasai na wakamba.Mkoa wa Kilimanjaro una wilaya 7 ambazo ni: HaiMoshiMwangaSihaRombo na Same.

                    HISTORIA YA MJI WA MOSHI
Kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012, mji huu una wakazi wapatao 184,292 [1]. Kabila linaloongoza kwa idadi ya wakazi wa mji wa Moshi ni Wachagga wakifuatiwa na Wapare na makabila mengine yaliyohamia kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania kamaWasambaaWarangi n.k. Wachagga wanapenda vyakula vinavyopikwa kwa kutumia ndizi kama vile mtorikitawa, na machalari.
Wakazi wengi wa Moshi ni wakulima, wafugaji na wafanyabiashara. Watu wengi wanaenda Moshi kufanya kazi na kurudi nyumbani jioni.
Ukuaji wa mji wa Moshi hauendani na mipango halisi ya 'Mipango Miji'. Hii inatokana na kutokufuatiliwa kwa sheria mbalimbali zinazohusu uendelezaji wa miji.

Hali ya Hewa

Moshi ni mji wenye baridi katika miezi ya Juni mpaka Agosti na kipindi cha joto katika miezi ya Oktoba hadi katikati ya Januari.

Utalii


Mji wa Moshi una mandhari nzuri ya kuvutia watalii. Watalii hupenda sana mji wa Moshi kwa sababu ya mlima Kilimanjaro na huduma muhimu kama mahoteli na usafiri.

Utawala


Kiutawala mji wa Moshi ni wilaya ya Mkoa wa Kilimanjaro. Ndani yake kuna kata 15 ambazo ni BondeniKaloleni,KarangaKiboroloniKiusaKorongoniLonguoMajengoMawenziMji MpyaMsarangaNjoroPasuaRauMfumunina Kilimanjaro. --41.222.183.59 13:58, 2 Agosti 2013 (UTC)

Elimu




Mji wa Moshi una vyuo vikuu vitatu:

  • MUCCoBS (Moshi University College Of Cooperative and Business Studies) ambacho ni chuo kikuu kishiriki chaSokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro
  • MWUCE (Mwenge University College Of Education) ambacho ni chuo kikuu kishiriki cha SAUT (St. Augustine University - Mwanza)
  • KCMC Medical School chini ya Chuo Kikuu cha Tumaini
  • O.U.T(The Open University of Tanzania) ambacho ni tawi la chuo chenye jina hilohilo chenye makao yake mkuu jijini Dar es salaam.
  • Historia ya Wapare


  • Kabla ya kuingia hapa nchini, inasemekana walikuwa Taveta, Kenya, kwa zaidi ya karne moja iliyopita na wakati huo walikuwa wakijulikana kwa jina la Waasu.

    Simulizi zinasema walipoingia Tanganyika, walitamani kufanya makao yao kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro, lakini wakavurumishwa na wenzao waliokuwepo hapo kabla yao, yaani Wachagga.
    Wachagga hawa hawakuwa radhi kuwaruhusu Wapare hawa kuwa na makazi eneo hili, hivyo waliwafukuza kwa kupigana kama ilivyokuwa tabia ya makabila mengi hapo zamani.Wakati wa kupambana walikuwa wakiambiana, “mpare…mpare” wakimaanisha ‘mpige…mpige!’Waasu hawa wakatimka mbio na kuparamia milima ambayo sasa inaitwa milima ya Upare. Waasu wakaanza kuitwa Wapare kwa maana ya "wapige".

    Hizi ni hadithi zinazosimuliwa na baadhi ya Wachagga ambao ndiyo watani pekee wa Wapare, utani uliozaliwa baada ya purukushani hizo za kuingia Tanganyika. Hata hivyo, hakuna hata Mpare mmoja anayeafiki maelezo hayo isipokuwa wanakiri kuwa walitokea Taveta ndiyo maana hata baadhi ya maneno na lafudhi yao haiko mbali sana na watu wa Taveta.
    Wapare wamegawanyika katika makundi mawili makubwa; wapare wa Pare ya Kusini ambao ni wapare wa Same na Wapare wa Pare ya Kaskazini ambao ni wapare wa Mwanga ambao na wao pia wamegawanyika mara mbili wapare wa Ugweno (wanatumia lugha inayoitwa Kigweno) na Wapare wa Usangi (Wanatumia lugha inayofahamika zaidi kama Kipare ambayo inatumiwa pia na wapare wa pare ya kusini ingawa inatofautiana kidogo katika matamshi.
  • Wapare wanatokea katika wilaya za Same na Mwanga, mkoa wa Kilimanjaro, lakini pia wapo katika wilaya ya Moshi Vijijini sehemu za Kahe, Chekereni, Himo, Mabungo, Moshi mjini, na pia katika wilaya ya Hai sehemu za Rundugai na mto Weruweru. Wapare pia wanaishi katika wilaya ya Lushoto, sehemu za Bumbuli na Mavumo. Wapare wanasemekana wametoka katika nchi ya Kenya sehemu za Taita, Taveta na Ukamba. Ni kabila la watu wachache lakini wana ushawishi mkubwa katika nyanja za siasa na uchumi wa Tanzania[onesha uthibitisho]. Wapare ni miongoni mwa makabila ambayo watu wake wamesoma sana. Wapare pia ni kabila la watu wanaopenda haki (yaani hawapendi kuonewa wala kumuonea mtu).Ndio maana watu wengine wanadhani wanapenda kesi,bali kesi ni njia mojawapo ya kuhakikisha haki inatendeka katika jamii. Dhuluma kwa Wapare ni kitu kilichokuwa kimepigwa marufuku hata kwenye matambiko yao, japo siku hizi kuna uwezekano baadhi yao wakawa hawana sifa hii tena.
  • Jamii za Wapare zimegawanyika katika makundi ya Wafugaji na Wakulima. Wakati Wafugaji wengi walihamia katika tambarare za Upareni, Wakulima wao waliishi milimani na wafuaji wa vyuma walikaa maeneo yote yaliyokuwa na uwezekano wa kupata chuma. Kwa asili Wapare hupeleka vijana wakiume jando (mshitu) ambako walipata mafunzo jinsi ya kuishi na familia,japo siku hizi tamaduni za kupeleka vijana mshitu hufanywa na watu wachache. Hata hivyo wapare wa Mwanga wamegawanyika katika jamii mbili: Wasangi na Wagweno. Wakati wasangi wanaongea kipare kinachoongelewa pia na Wapare wa maeneo mengine, Wagweno wao wana lugha yao iitwayo Kigweno. Kigweno ni mchanganyika wa Kipare na Kichagga. Hii inaonesha kuwa asili ya Wagweno ni uchagani. Hata hivyo mila na desturi za Wagweno zinafanana zaidi na zile za wapare wengine. Wapare ni wachapakazi sana wakichanganya kilimo, ufugaji na biashara, ndio maana hata leo wana uchumi mzuri katika viwango vya Tanzania. Zamani Wapare walikuwa na sala tofauti,kwa kila koo na eneo lao la tambiko, katika karne ya 19 hadi 20 wamisherani wa Kikiristo waliingia maeneo mengi ya Upare.
    Wapare walianza kufua chuma kabla ya mwaka 1700 na wafuaji walikuwa wakiitwa Washana, na huo ukoo upo hata leo hii. Wapare walikuwa wakiuza bidhaa zinazotengenezwa na chuma kama majembe,mapanga, visu, silaha kama mikuki kwa makabila ya jirani mfano Wachaga,na wamekuwa na uhusiano tangu siku nyingi. Bidhaa zao hizi ziliuzwa hata kwa Wasambaa.

  • Mzee Katengu Ramadhani ni Mpare. Anasimulia kuwa Wapare ni kabila lenye ujasiri na ni watu wa kupanga kabla ya kutenda. Pia anaongeza kuwa ni wavumilivu wenye kustahimili hali ngumu ya maisha ikiwa ni pamoja na njaa au kutokuwa na pesa.Inasemekana Wapare kwa ujasri mkubwa enzi za ukoloni waliweza kujiunga pamoja na kufanya mgomo wa kukataa kodi za kikoloni zilizokithiri. Mgomo huo uliofanikiwa ulijulikana kama ‘mbiru’. Hata hivyo, nilivutiwa zaidi alipozungumzia mfumo wa maisha waliokuwa ambao kwangu niliuona ni wenye kuwaongezea sifa katika nchi hii.
    Mzee Katengu Ramadhani alisimulia kuhusu mila na desturi ya Wapare zilizowajengea taratibu za kuwa na mifumo waliyoiita ‘Ndala’, ‘Msaragambo’ na ‘Kiwili’.Kwa mujibu wa mzee huyo neno ‘ndala’ kwa Kipare humaanisha utaratibu wa familia au watu wanaoishi jirani mno kuwa na tabia ya kula chakula kwa pamoja, kama wengi tuonavyo waislamu waliofunga na wanapofuturu pamoja.
    Utaratibu wa Wapare ulikuwa kwamba kila mama anapotayarisha chakula kwa familia yake, ilibidi akitoe achanganye na chakula kingine cha wenzake na familia zote ziketi na kula pamoja. Mfumo wa ndala kwa maana ya familia kula chakula kwa pamoja unaonekana kuwa na manufaa yafuatayo. Kwanza unajenga mahusiano mema baina ya familia na majirani katika kushirikiana. Pili kushirikiana katika kula kunachochea ushirikiano katika mambo mengine kama shida au raha. Lakini pia watoto wanaokuzwa katika mfumo huo wanajengwa katika maadili mazuri wasiwe walafi na wachoyo maana wanazoea kuwa na wenzao na hii ndiyo sababu kabila hili lilikuwa na sifa ya kuwa wakarimu.
    Watoto walifundishwa kuwa na nidhamu ya wakati wa chakula, kwa mfano kutonawa mikono au kuanza kula kabla ya wakubwa.Neno msaragambo linamaanisha mfumo uliokubaliwa na jamii katika kitongoji, kijiji au kata wa kushirikiana katika kufanya kazi zenye faida kwa watu wote, maarufu kwa kazi za ujenzi wa taifa.
    Kwa kazi hizi ni za ridhaa zilipaswa kwanza zikubaliwe na wengi vinginevyo haikuwa rahisi mtu mmoja kuitisha wito wa kazi fulani na watu wengine kuja kuifanya. Kazi hizi ambazo hata serikali ya awamu ya kwanza ilizikazania sana mara baada ya Tanganyika kupata uhuru, ni pamoja na ujenzi wa mashule, kuchimba visima vya maji, kuchimba barabara na kadhalika. Upo ushahidi wa kutosha kuhusu Wapare walivyotumia mfumo huu na kupata maendeleo makubwa Wilayani mwao.
    Zipo barabara za Mwanga hadi Ugweno na Usangi; Ndungu hadi Mamba na Vunta; Hedaru hadi Mwala; Makanya hadi Chome,Mpirani hadi Bombo Song’ana,Gonja Maore hadi Vuje naVudee hadi Mbaga. Hata hivyo, si barabara tu lakini zahanati, na shule nyingi zimejengwa na wapare wa wilaya za Same na Mwanga na kuinua kiwango cha maendeleo yao.
    Nakumbuka watu hawa si watu wapenda misaada ya mteremko ndiyo maana pamoja na kukabiliana na hali mbaya ya uhaba wa mvua mara kwa mara wamekuwa si watu wa kupiga yowe haraka. Kazi zilizofanywa kupitia utaratibu huu wa msaragambo ziliufanya Mkoa huu wa Kilimanjaro uongoze kwa maendeleo ya barabara nzuri, ujenzi wa shule nyingi hadi katika vitongoji.Kiwili ni msamiati mwingine wa Kipare ambao ni mfumo wa maisha walioukubali katika kuendesha maisha ya familia na jamii zao kwa kusaidiana kazi.
    Kiwiri ni utaratibu ambapo familia au majirani hualikana ili kusaidiana katika kazi za kilimo, na hata mavuno hasa pale mmoja wao anapokuwa na kazi shambani mwake na kuhitaji msaada. Siku hiyo, watu hukutana na kufanya kazi hiyo waliyoitiwa, mwenye kazi huandaa chakula ambacho watu watapata baada ya kumaliza kazi.
    Utaratibu huu ulikuwa na manufaa makubwa maana ulirahisisha kazi na kujenga moyo wa kusaidiana. Kiwiri pia kiliweza kuitishwa na majirani kuwalenga wazee waliochoka au wagonjwa, ambao kwa namna moja au nyingine walionekana kushindwa kumudu kazi zao za shambani. Kupitia kazi za kusaidiana maisha ya familia nyingi za Wapare ziliokolewa na majanga ya kufikwa na njaa.
    Bilashaka utakuwa umebaini kuwa zipo mila na desturi nzuri ambazo Watanzania tulikuwa nazo, lakini wageni wakatuhadaa na kutulaghai kwamba ya kwetu yote yalikuwa si mema nasi tukaanza kuyaacha.Imani za Wapare kwa sasa zinatofautiana kutokana na maeneo, walio Kusini mwa wilaya ya Same katika maeneo ya Ndungu,Kihurio,Bendera,Hedaru,Makanya,Suji,Chome,Tae,Gonja, Mamba hadi Vunta kuna waumini wa kanisla la Sabato wengi sana,maeneo kama Chome,Mbaga,Gonja, Vudee yana waumini wengi wa kanisala la Kiluteri, Katika Wilaya ya Mwanga kuna idadi kubwa ya Waluteri na Waislamu. Wakatoliki, japo ni wachache, wanapatikana zaidi katika maeneo ya Kisangara juu, Vumari,Kighare na Mbaga.Makande (Mpure),ugali(hasa ule wa muhogo wanauita ibadaa), ndiziwali kwa wale wanaoishi maeneo ya tambarare kama Ndungu, Kisiwani, Maore na Mpirani. Pia kuna vyakula kama Kishumba, Kibulu, na mboga maarufu "Msele" nkokoro n.k
    Wapare pia wana ukaribu na makabila ya Mkoa wa Tanga hasa Wasambaa, Wazigua na Wanguu. Ukaribu wao uko katika lugha ambapo maneno mengi ya makabila haya yanafanana. Vile vile hata majina ya baadhi ya maeneo yaliyopo kwa Wapare yapo pia kwenye maeneo wanamoishi makabila kama vile Wasambaa na Wanguu. Kwa mfano, kwa Wapare kuna majina ya maeneo kama vile Gonja, Ndeme, Ndolwa n.k. Majina haya yapo pia maeneo ya Wanguu na Wasambaa. Hii inaonesha kwamba makabila haya yana asili moja.
  • Maeneo mazuri ya kutembelea

    • Mbuga ya Mkomazi
    • Bwawa la Nyumba ya Mungu
    • Msitu wa asili wa Shengena
    • Bwawa la Kalimawe
    • Maporomoko ya Ndurumo - Gonja Bombo
    • Msitu wa Ngagheni Mpinji- Vudee uliokuwa wa matambiko karne ya 17 mpaka 19
    • Mlima wa Masheko Ndolwa-Vudee uliokuwa na Matambiko ya Wapare
    • Jabali la Mhewe -Vudee lililopasuliwa na wananchi wa Vudee kuwezesha barabara kupita miaka ya 1960 na 1961.
    • Msitu wa Wambugu ulioko karibu na Dangaseta- Mwembe uliotumika kwa matambiko ya kabila linaloishi Lushoto Tanga-hadi leo wachache wao bado hufika kutambika pale.
    • Kulikuwa na imani potovu kuwa mwanamke akizaa watoto mapacha analeta mkosi na laana kwenye ukoo pia mtoto akianza kuota meno na yakaanza kuotaa ya juu,kwa hiyo watoto hao waliuawa kwa kutupwa au huegeshwa juu kilele pembezoni wakiwa wamelala baada ya kunyonyeshwa ama kulishwa uji na wazazi wao kwenye jiwe kubwa ambalo kule Mbaga - Pare ya kusini linaitwa Malameni, Usangi - Mwero linaitwa Ikamba pia na Mfinga ya Kikweni makutano ya kwenda Ugweno na Usangi linaitwa Lubegho ambapo ni aghalabu mtoto kupona kwani akiamka toka usingizini akijigeuza tu hudondoka toka kule ju hadi chini nakufa. Maajabu ni kwa mtoto mmoja aliye okotwa na Mzee Mgaya kule Ikamba na kumlea hadi akakuwa na kuwa Mtumishi wa Mungu jasiri na maarufu Marehemu Mchungaji Nathanaeli Mgaya. Hadi leo hii mawe hayo yapo.Kuna mto Yongoma, Hingilili, Mhoke vuta, Nakombo, Rika, Mweta nano hii mito yote iko Pare ya kusini. Katika mto Hingilili kuna maporomoko makubwa na yanayosadikiwa kuwa marefu kuliko yale ya Victoria Falls, haya yanajulikana kama Ndurumo yapo eneo la Gonja Bombo umbali wmfupi kutoka mtaa wa Mang'ang'a katika eneo linaloitwa Mbula.Kuna ziwa Jipe, bwawa la Nyumba ya Mungu na Kalemawe n.k
    • Watu mashuhuri wa Upare

      • Chedieli Yohane Mgonja aliwahi kuwa Mbunge na waziri wa Elimu katika serikali ya awamu ya kwanza
      • Cleopa David Msuya bado yupo hai na aliwahi kuwa waziri wa Fedhawaziri mkuu
      • Mfumwa Singo
      • Askofu Eliewaha Eliya Mshana]]
      • Anne Kilango mbunge wa Same mashariki
      • Asha-Rose Mtengeti Migiro aliyewahi kuwa naibu katibu mkuu wa UN
      • Mathayo David mbunge wa Same Magharibi na Waziri
      • Peter Kisumo
      • Daktari Mbazi Fikeni Senkoro
      • Mchungaji Abrahamu Itunda
      • Felix Mlaki mchumi maarufu na mtu wa benki anamiliki kampuni za ushauri na mikopo
      • Profesa Jumanne Maghembe Waziri wa Maji
      • Mfumwa Sabuni wa Usangi
      • Mfumwa Manento Sekimanga wa Mamba
      • Joseph Mamphombe wa Mbaga
      • Kigono Chuma wa Gonja
      • Folong'o Makange wa Chome
      • Minja Kukome wa Ugweno
      • Yoeli Mtindi wa Hedaru
      • Mfumwa Njaule wa Vudee, IGP wa kwanza baada ya uhuru
      • Elangwa Shaidi wa Vudee
      • Mchungaji Kadiva Ernest William wa Hedaru/Chome, Naibu Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani na mbunge wa Bunge Maalum la Katiba Tanzania
      • Professor Joseph Semboja ambaye ni mchumi na mkuu wa Taasisi ya Uongozi iliyo chini ya ofisi ya Rais
      • Wachagga


      • Wachagga ni kabila la watu wenye asili ya Kibantu wanaoishi kaskazini mwa Tanzania chini ya mlima Kilimanjaromkoani Kilimanjaro. Shughuli kubwa ya Wachagga ni biashara nakilimo.

        Wachagga ni kabila la tatu kwa ukubwa nchini Tanzania. Takwimu za mwaka 2003 zinaonyesha kuwa idadi ya Wachagga mkoani Kilimanjaro ni 200,000.
        Lugha ya Kichagga, inabadilika kuanzia unapotoka Tarakea mpaka unapofika Siha magharibi mwa Kilimanjaro. Kutokana na tofauti hizo Kichagga kimegawanyika katika Kirombo,KimaranguKi-Old Moshi,KikiboshoKimachameKikirua na Kisiha. Lugha hizi zinakaribia kufanana kulingana na jinsi makabila hayo yalivyopakana. Kwa mfano, Ki-Marangu kinafanana na Kikirua. Vile vile Kisiha kinafanana sana na Kimachame ambacho pia kinafanana kidogo na Kikibosho. Baadhi ya Wamachame walihamia sehemu za Meru Arusha na kuchanganyikana na Waarusha, lugha yao ikabadilika kidogo na kuwa Ki-meru. Kwa sababu hii Wameru wanasikilizana sana na Wamachame ingawa lafudhi zao zinatofautiana kidogo.

          • Wachagga wanajulikana kwa uwezo wao mkubwa wa kufanya biashara na pia kilimo. Moshi ni maeneo ya mwanzo ambayo Wamisionari wa Kikristo walijenga makanisa na shule. Sababu hii imefanya Wachagga kuwa kabila lenye watu wengi zaidi walio na elimu ya kisasa na mkoa wa Kilimanjaro unaongoza kwa idadi ya shule za sekondari nchini Tanzania. Kulingana na takwimu za elimu mkoa wa Kilimanjaro una shule za sekondari zaidi ya 320. Pia mkoa una shule za msingi zipatazo 950. Idadi hii ya shule ni kubwa zaidi ya idadi ya shule katika mikoa mingine Tanzania.
        Shule nyingi za sekondari ziko katika mkoa huu kwa sababu zifuatazo: 1) Hali ya hewa na vivutio vya kitalii katika mkoa huu viliwavutia zaidi walowezi na wakoloni na kuweka makazi yao hapo. Hivyo wamishinari walijenga shule za kwanza wakifuatiliwa na serikali za wakoloni 2) Serikali ya Tanzania ilirithi shule zilizojengwa na wakoloni 3) Wachagga waliobahatika kupata fedha binafsi baadaye waliwekeza kwenye ujenzi wa shule binafsi kama kitega-uchumi. Wakati wakazi wa mikoa mingine walisubiri serikali iwajengee shule. 4) Ukichanganya sababu 1,2 & 3 utagundua shule katika mkoa Kilimanjaro vimezidi sana idadi ya shule katika miko mingine yote.
        Ni vema pia kusema kwamba shule hizi kuvutia wanafunzi kutoka Tanzania nzima, haziwasomeshi wachagga tu.

          • ngawa wachaga wa leo wanakula vyakula mbali mbali kama vile ugaliwali na viazi, chakula kikuu cha Wachagga ni ndizi. Kuna ndizi za aina mbalimbali na hutumika kwa matumiza tofauti. Mfano ndizi kisukari ni fupi na huachwa hadi ziive na huliwa mbivu kama tunda. Ndizi mshare kukatwa zikiwa mbichi na kupikwa chakula mbalimbali pamoja na nyama ya ngombe, kondoo au mbuzi. Mara nyingine hupikwa na maharage, choroko,kunde au hata maziwa ya mtindi. Vyakula vya ndizi huja kwa ladha tofauti kama vile ndizi nyama, mtori, machalari, kiburu na kadhalika.
        Aina nyingine ni ndizi-ngombe ambazo huachwa ziive halafu humenywa na kutumiwa kutengenezea pombe maarufu iitwayo mbege. Mbege hutengenezwa kwa kutumia ndizi mbivu, maji, na ulezi.
        Aina nyingine ni ndizi-mzuzu. Hizi zikikomaa huachwa zianze kuiva kidogo halafu huchomwa na kuliwa kama kitafunwa pamoja na chai au pombe. Ukipita mitaa ya Darisalamu utaona ndizi- mzuzu zikichomwa sambamba na muhogo au kuku-vumbi au kiti-moto.
        Inasemekana kuwa "mchagga halisi, hali muhogo - akila muhogo atakufa". Usemi huu umetokana na historia ya mababu kuwa wachagga waliopanda mihogo Kilimanjaro enzi za kale walikufa baada ya kuila. Historia hiyo yaweza kuwa ya ukweli kwa sababu aina nyingi za mihogo zinajenga sumu ya sianidi ndani yao; watu waliozoea kutumia mihogo huwa na njia za kuondoa sumu kwa kwa kuiloweka mihogo katika maji kwa muda. Lakini kama Wachagga wale wa zamani hasa wa Machame walifanya jaribio bila kujua mbinu ya kuondoa sumu ajali iliweza kutokea. Cha kushangaza ni kwamba huko huko Kilimanjaro, majirani na watani wa wachagga yaani Wapare walikuwa wameshazoea mihogo na ilikuja kuwa moja ya chakula chao kikuu.Pamoja na kilimo cha mazao, wachagga hupendelea sana kufuga nguruwe. Tabia ya kula nyama ya nguruwe ijulikanayo leo kwa jina la "kiti moto" ni moja ya mambo yaliyoenezwa na wachagga. Ulaji wa "kiti moto" haukupendeza baadhi ya wenyeji wa Pwani kama Dar es Salaam ambapo wachagga walihamia, kwani wakaaji wengi wa Pwani ni Waislamu kwa hiyo nguruwe kwao ni haramu. Wakazi wa Dar es Salaam watokao makabila mengine na wasiyo waisalmu kwao kula nguruwe ilikuwa "ruksa".

          • Majina ya kiukoo ya Kichagga pia huashiria wanatoka sehemu gani ya Uchaga, japo si lazima kuwa hivyo: mfano familia maarufu za Kichagga nchini Tanzania ni kama ukoo wa akina Mushi,Kimaro, Swai, Massawe, Lema, Urassa, Nkya, Ndosi, Meena hutoka Machame. Akina Temu, Mlaki, Mlay, Lyimo, Moshiro, Mselle, Kileo, Kimambo, Tesha wanatoka Old Moshi na Vunjo. Kavishe,Mariki, Tarimo, Laswai, Mallya, Mrema, Mkenda, Massawe,silayo, Lyaruu, Makyao, Mowo, Lamtey, Tairo, Mramba, Kauki wanatoka Rombo. Sawe, Usiri, Shayo, Kiwelu, Makundi, Urasa, Mtui, Moshi, Meela, Minja, Njau wanatoka Marangu na Kilema. Rite, Makule, Minja, Mashayo, Chao, Shao, Makawia, Ndesano, Kimario, Tilla, Mariale, Tarimo, Mafole, Kituo, Mrosso, Lyakundia, Kessy, Mmbando, Matemba, Ndenshau, Morio, Akaro, Matowo, Towo, Mkony, Temba Foya,na kilawe na kadhalika hutoka Kibosho.Ukoo wa akina Teri wako Mamba Kiria na wachache Sango, Old Moshi na wengine walihamia Maji ya Chai, Mkoa wa Arusha.
        Wachagga wengi hupenda kurudi nyumbani kipindi cha Krismasi, ikiwa ni kuwatembelea wazazi wao, rafiki, au ndugu. Ingawa wengi hudhani kwamba Wachagga wameathiriwa sana na dini ya Ukristo kwa kuwa wengi wao ni Wakristo na hiki huwa ni kipindi cha likizo kwao, inaaminika pia kuwa kurudi kwao Uchagani wakati wa Krismasi ni pamoja na kutembelea ndugu zao na kujumuika pamoja katika kuumaliza mwaka baada ya kazi nyingi za kutafuta pesa kwa mwaka mzima.

          • Watawala wa kichagga waliitwa "Mangi". Hawa walihodhi mashamba, ngombe na waliheshimiwa kama viongozi wa kikabila. Walikuwa na nguvu za kisiasa na utajiri. Baadhi ya ma-mangi mashuhuri katika historia ni kama Mangi Rindi aliyeingia mikataba na wakoloni (wajerumani), Mangi Sina wa kibosho - anajulikana kwa uhodari wake wa vita katika kupigana na wamachame na kupora ngombe na mazao yao na Mangi Marealle wa Marangu na Vunjo. Wakoloni walipokuja Kilimanjaro waliingia mikataba na viongozi hawa wa kikabila ili kuweza kuweka misingi yao ya kikoloni. Pia ndugu na watoto wa ma-Mangi walikuwa wa kwanza kupata elimu ya kikoloni, kwa hiyo waliweza kushirikishwa katika serikali za kwanza. Hawa pia wanaaminika walikuwa ni kama mabepari wa kwanza wa ki-jadi, maana walifanyiwa kazi na watu wengine wakati wao ma-mangi wamekaa kuhesabu mali zao. Usemi maarufu wa "u-Mangi-meza" nadharia
        inawezekana kuwa umetokana na watawala hawa wa kichagga.

          • Ingawa ardhi ni msingi wa maendeleo kwa watu wote, kwa wachagga, ardhi ni mali sana kwa sababu kilimo chao ni cha mazao ya kudumu kama kahawa na ndizi hukaa shambani kwa muda wa miaka mingi. Mojawapo ya urithi wapewayo watoto ni "kihamba". Hii ni sehemu ya ardhi ambayo mtoto anategemewa atajenga na kuanzisha familia yake. Bahati mbaya watoto wa kike walikuwa hawapewi kipaumbele katika ugawanaji wa vihamba. Uhaba wa ardhi uchagani ulipelekea wachagga wengi kuhamia mikoa mingine. Hivi leo utakuta wachagga wakiishi Dodoma, Morogoro, Iringa, Mbeya nk wakiwa wamepanda migomba yao na kuendesha biashara za maduka ya vyakula. Ukienda kwenye mikoa hii utakuta wamejenga jamii zao na vyama vyao vya kusaidiana wakati wa sherehe au matatizo. Aidha hata pombe ya mbege utaweza kuikuta katika makusanyio ya wachaga mikoani mbali mbali.Ingawa wanaume wa kichagga hupendelea kufanya kazi mbali na kwao, wake zao hukaa nyumbani (Moshi) na hufuga ngombe na kazi za shambani. ila kwa sasa kutokana na ugonjwa wa ukimwi tabia hii imepungua miongon mwao. Wanawake wa kichagga (hasa kutoka Rombo) hujulikana kama wafanyakazi hodari. Huchangia sana katika mapato ya nyumbani na chakula. Ingawa kipato cha wachaga ni kikubwa kulinganisha na cha makabila mengine, takwimu zinaonyesha watoto wa mkoa wa Kilimanjaro kuwa kuongoza kwa utapiamlo. Sababu kubwa ya watoto kuwa na utapiamlo kunatokana na wazazi kujali zaidi kazi kuliko muda wa kuwahudumia watoto. Wengi wa wototo ni wale ambao wazazi wao ni watu wapombe na kipato chao kinaishia kilabuni. Utaona kwamba uchagani kuna vilabu vingi vya pombe na vinaongezeka kwa sababu imekuwa nibiashara kubwa. Karibu kila kaya kumi natano kuna kila cha pombe na kiwango cha chini kabisa cha pombe inayouzwa kwa siku katika vilabu hivyo si chini ya dede sita au lita mia moja. Pombe ni sababu moja ya watoto kuwa na utapiamlo Hii inawezekana kuwa matunda ya wazazi kutowalisha watoto wao chakula cha kutosha au chakula bora. Kuna sehemu nyingine za Uchaggani kama Old Moshi na Kibosho ambapo watoto wadogo hupewa pombe ya mbege asubuhi mchana na jioni. Sababu nyingi ni kazi; mama wa kichagga anaweza kushinda shambani kutwa na hawana desturi ya kubeba watoto mgongoni kwenda nao shambani hivyo wanakuwa nyumbani ama wenyewe au na mayaya. Mfano ulio dhahiri ni nyakati za asubuhi na mapema kwenye vyombo vya usafiri karibu robo tatu ya abiria ni wanawake wakienda katika shuguli za kibiashara na kilimo na vivyo hivyo nyakati za jioni wakirudi majumbani. Hao ni nje ya wale wanaotumia usafiri wa miguu ambao ni wengi zaidi. Pia baadhi ya wamama wa kichaga wanawajali waume zao zaidi kwani nyama nzuri ni ya baba. Kuepuka gharama baba ataandaliwa chakula kizuri tofauti na chakulawalichoandaliwa watoto japo ni chakula kilekile.pia wachaga wamekua na desturi ya kuwaenzi wazee wao walio tangulia mbele za haki kwa kuwatambikia kwa pombe na nyama za mbuzi pale tu wanapo rudi nyumbani ifikapo mwezi desemba. hili limekua ni swala la kawaida sana na halipingiki. wengi wao huwa wanarudi na magari ndio sababu utaona ya kwambwa kila ifikapo mwezi desemba kila mwaka foleni za magari zimekua zikiongezeka kutokana na wachaga kurudi nyumbani msimu wa sikukuu. wengi wao wamekua wakitoka sehemu mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi Wachaga wazamani ndo huacha wake migombani.mimi niko na wa kwangu hapahapa